Ufunuo wa Yohana Mlango 12 Revelation

Ufunuo wa Yohana 12:1 Revelation 12:1

Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili.

Ufunuo wa Yohana 12:2 Revelation 12:2

Naye alikuwa ana mimba, akilia, hali ana utungu na kuumwa katika kuzaa.

Ufunuo wa Yohana 12:3 Revelation 12:3

Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.

Ufunuo wa Yohana 12:4 Revelation 12:4

Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.

Ufunuo wa Yohana 12:5 Revelation 12:5

Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi.

Ufunuo wa Yohana 12:6 Revelation 12:6

Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko muda wa siku elfu na mia mbili na sitini.

Ufunuo wa Yohana 12:7 Revelation 12:7

Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

Ufunuo wa Yohana 12:8 Revelation 12:8

nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.

Ufunuo wa Yohana 12:9 Revelation 12:9

Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

Ufunuo wa Yohana 12:10 Revelation 12:10

Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.

Ufunuo wa Yohana 12:11 Revelation 12:11

Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

Ufunuo wa Yohana 12:12 Revelation 12:12

Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.

Ufunuo wa Yohana 12:13 Revelation 12:13

Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

Ufunuo wa Yohana 12:14 Revelation 12:14

Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.

Ufunuo wa Yohana 12:15 Revelation 12:15

Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.

Ufunuo wa Yohana 12:16 Revelation 12:16

Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.

Ufunuo wa Yohana 12:17 Revelation 12:17

Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.